Wednesday, 24 October 2018

USHUHUDA.


Shalom Mtumishi, juzi baada ya kufundisha somo kuhusu malaika niliingia kwenye maombi na baada ya maombi nililala nikaota ninapanda mlima halafu nikashindwa kupanda ile nilishakata tamaa ya kupanda wakaja watu wawili mmoja nyuma yangu na mwingine mbele, wa mbele akanishika mikono na wanyuma akanishika miguu na nikapandishwa ule mlima .

Jana pia nilisoma somo uliyofundisha jinsi ya kupigana vita ya kiroho, na nikaona yale maombi uliyoandika katikati ya somo kuhusu maadui kuwekea alama na kisha Malaika akiwaona wawapige. Baada ya kuomba niliota ndoto niko sehemu ninapita kwenye ukuta mrefu sana na nikajikuta kuna kitu kimenipaisha juu sana nikawa ninatembea juu juu tu hadi nikamaliza ule ukuta nikatua sehemu safi.

No comments:

Post a Comment

KAZI KUU TANO (5) ZA IMANI KATIKA MAOMBI.

Bwana YESU atukuzwe ndugu zangu. Karibu tujifunze Neno la MUNGU. Uhusiano ni upendo unaozaa ushirikiano na mawasiliano kati ya pande m...