HUDUMA TANO TEULE.
*WAEFESO 4: 11 – 14.*
*11 Naye alitoa wengine kuwa mitume, na wengine kuwa manabii; na
wengine kuwa wainjilisti na wengine kuwa wachungaji na waalimu; 12 kwa
kusudi la kuwakamilisha watakatifu, hata kazi ya huduma itendeke, hata
mwili wa Kristo ujengwe; 13 hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa
imani na kumfahamu sana Mwana wa Mungu, hata kuwa mtu mkamilifu, hata
kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo; 14 ili tusiwe tena
watoto wachanga, tukitupwa huku na huku, na kuchukuliwa na kila upepo wa
elimu, kwa hila ya watu, kwa ujanja, tukizifuata njia za udanganyifu.
Katika maandiko yote katika bibilia ambayo yanazungumzia huduma
ambazo Mungu kupitia Yesu Kristo amezitoa na kuziweka ndani ya Kanisa,
hili ni andiko la pekee ambalo linataja huduma zote tano na majukumu
yake ya ujumla ndani ya mwili wa Yesu Kristo.
Sasa yapo maandiko mengine mengi ambayo yanataja huduma mojawapo au
baadhi ya hizo ambazo zimetajwa kwenye hili andiko lakini hili andiko
ambalo tumenukuu ndo andiko la pekee ambalo zote zimetajwa kwa pamoja
alafu majukumu yake ya jumla kwa pamoja yakaainishwa hapa.
Ili kuweza kujua kama mtu anayedai kuwa yeye ni huduma fulani, pamoja
na kujua mambo muhususi yanayohusu hiyo huduma kama ambavyo
yameainishwa katika maandiko sehemu nyingine katika bibilia ni muhimu
sana ujue haya majukumu ya jumla ya huduma zote na kama katika utendaji
wake pamoja na hivyo vya kipekee kwa huduma husika anayodai yeye ni,
lazima hizi hapa zilizotajwa awe anafanya kwa kushirikiana na huduma
hizo zingine.
Maandiko yanatuambia kuwa alitoa wengine kuwa mitume, na wengine kuwa
manabii; na wengine kuwa wainilisti na wengine kuwa wachungaji na
waalimu.
Hii sentensi ilivyokaa imepelekea wengine kusema kuwa zipo huduma nne na mimi sitofautiane nao sana.
Ni kweli sentensi ilivyokaa inaonyesha wazi kabisa kuwa kuna huduma zifuatazo:
*1. Mitume.*
*2. Manabii.*
*3. Wainjilisti.*
*4.Wachungaji na Waalimu.*
*2. Manabii.*
*3. Wainjilisti.*
*4.Wachungaji na Waalimu.*
Katika pita pita yangu nimeona wachungaji wasio waalimu na nimekutana
pia na waalimu wasiyo wachungaji na imenipelekea kuamini kuwa zipo
tano.
Lakini pia wale wanaosema zipo nne hawajakosea pia kutokana na mantiki ya jinsi hiyo sentensi ilivyotungwa.
Sasa maandiko yanaanza kuainisha majukumu ya jumla na ya pamoja ya hizi huduma (ziwe tano au nne haina shida kabisa).
*i).* Hizi huduma kwa pamoja zinawakamilisha watakatifu hata kazi ya huduma itendeke.
Kuna tafsiri zingine zinasema kuwa zinawaandaa watakatifu kwa ajili ya kufanya kjazi ya huduma.
Kuna tafsiri ambazo zinasema kuwa zinaweka mikononi mwa watakatifu vitendea kazi ili kazi ya huduma itendeke.
Wito wa kuifanya huduma sio kwa ajili ya watu wachache waliyo na mmojwapo ya hizi huduma ambazo zimetajwa.
Wito wa kufanya huduma ni kwa ajili ya kila mmoja wetu aliyeokoka.
Lakini wenye jukumu la kutuandaa Kanisa la Yesu Kristo kwa ajili ya
kufanya hizi kazi za huduma ni hawa wandugu waliyoitwa kwenye hizi ofisi
teule.
Kwa hiyo kama mtu ni mtume, au nabii, au mwinjilisti, au mchunagaji
au mwalimu, pamoja na majukumu ya kipekee yanayoendana na ofisi yake
lakini lazima atahusika katika kuwakamilisha watakatifu, kuwaandaa
watakatifu, na kuweka mikononi mwao vitendea kazi ili kazi ya huduma
itendeke.
Sio tu watawakamilisha watakatifu, kuwaandaa na kuweka mikononi mwao
vitendea kazi kwa ajili ya kufanya kazi ya huduma lakini pia ili mwili
wa Kristo ujengwe.
Moja ya vitu ambavyo vinaweza vikaanza kuleta mashaka katika madai ya
kuwa fulani ni mmojawapo ya huduma hizi teule ni ile yeye kujenga
Ufalme wake badala kujenga mwili wa Kristo.
Hili jukumu ambalo tumepewa kujenga mwili wa Kristo unatoa uhuru kwa
yeyeote kati ya hawa ambao wapo kwenye huduma hizi teule kuyasemea mambo
ambayo anaona ni hatari kwa ujenzi, ufanisi, mafanikio na ustawi wa
mwili wa Kristo.
Tukumbuke kuwa Kanisa sio la mtu awaye yeyote.
Kanisa ni la Yesu Kristo na kama kuna kitu hakijakaa sawa anaweza akamgusa mtu kuyasemea hayo kwa niaba yake.
Kumbuka Yesu alisema alipokuwa akiongea na Petro kuwa Yeye atalijenga Kanisa Lake na milango ya kuzimu haitalishinda.
Hata Paulo Mtume alithubutu kusema kuwa Yeye ni mjenzi stadi mwenye
hekima na akadai kuwa ameuweka msingi lakini kila ajengaye juu awe
makini sana anajengaje na anajenga kwa kutumia nini.
*ii).* Jukumu lingine la hizi huduma kwa pamoja na kwa ujumla kama
zilivyoainishwa na mistari ambayo tumetoka kuinukuu ni kulileta Kanisa
katika umoja wa imani na kumfahamu sana Mwana wa MUngu.
Dini na madhehebu haziwezi kutufikisha hapo.
Ni hizi huduma teule kwa kusimama kwenye nafasi zao kama walivyotolewa na Kristo.
Hizi huduma zinapotekeleza majukumu yao zitauleta mwili katika umoja wa imani na kumfahamu sana Mwana wa Mungu.
Kama Kanisa halikui katika kumfahamu sana Mwana wa Mungu na halikui
katika umoja wa imani basi hizi huduma teule hazitekelezi wajibu wao
ipasavyo.
Kama ni kakundi fulani tu kanajiona kenyewe kako bora kuliko sehemu
nyingine ya mwili wa Kristo basi hiyo ni hali iliyo kinyume na dhumuni
la kuuleta Mwili wa Kristo katika umoja wa imani na kumfahamu sana Mwana
wa Mungu.
Leo hii tumetengana sana kiimani.
Huyu anaamini hiki, yule kile.
Hii ni kwa sababu hatujafanya maandiko ndo msingi wa kuamini kwetu wote.
Mbaya zaidi yapo makundi ambao wanaamini vitu visivyo na mashiko katika maandiko.
Na hii imesababishwa na watu wanaodai kuwa wao ni mojawapo ya huduma hizi teule.
Hawa watiu wanadai kuwa Mungu aliwatokea na kuzungumza nao na
kuwafunulia lakini hicho wanachodai kuwa Mungu aliwatokea na kuwafunulia
kinakinzana na maandiko, na wakichanganyamo na tu muujiza uchwara na
twa uongo viwili vitatu watu wanawaamini alafu kanazaliwa kakundi ambako
kenyewe hakana ushirikiano na sehemu iliyosalia ya mwili.
Hii ni kinyume kabisa na jukumu hili ambalo tumelianisha la kuleta Kanisa katika umoja wa imani.
Leo hii watu wanawajua, kuwasikiliza, kuwaamini, kuwatii na hata
kuwataja wale wanaodai wao ni mojawapo ya huduma teule kuliko hata Yesu.
Kama tukiwa huduma teule tutaelekeza watu katika kumjua sana Mwana wa Mungu.
*iii).* Hizi huduma teule zitashirikiana kuleleta kanisa kuwa mtu mkamilifu na tena kwenye cheo cha utimilifu cha Kristo.
Ili hili liwezekane lazima hizi huduma pamoja na majukumu mengine
ambayo ni ya kipekee kwa huduma hiyo, zifundishe maana maarifa yanakuza
na kumfanya mtu azidi kuwa mkamilifu.
Katika utekelezaji wa haya majukumu ni ili Kanisa lisiendelee kuwa
watoto wachanga wanaotupwa huku na huku na kuchukuliwa na kila upepo wa
elimu ambazo kimsingi ni kwa hila za watu na ujanja huku tukifuata njia
za udanganyifu.
Kuna watu wengi sana ambao wanajiita watumishi ambao kimsingi ni watu wa hila tu, wajanja wajanja ambao wanadanganya watu.
Namna mojawapo ya kuwatambua ni je wanafanya haya yaliyoainishwa na hili andiko tulilonukuu?
No comments:
Post a Comment