Sunday, 15 July 2018

USHUHUDA.



Bwana Yesu asifiwe Mtumishi Peter Mabula nashukuru Mungu kwa maombi yako kuhusu kuota ndoto nafanya mapenzi na watu nisiowajua, nashukuru toka umeniombea zile ndoto azijanirudia tena wala kuota kuwa nafukuzana na wachawi tangu tumefanya maombi Mungu kanijibu kwakweli nashukuru kwa maombi yako bado tu suala Ka kupata kazi ndo nashuhulikia katika hilo nawatafuta watu wenye ofisi ili waweze kunisaidia kupata kazi kama nilivyokuambia kuwa sina MTU wa kunisomesha ndo nikipata hiyo kazi niweze kujiendeleza kimaisha na kimasomo.
Natumaini hata hili nalo litapita tu na huu mwezi wa saba hautaisha bila ya kujibiwa ombi langu la kupata ofisi Mungu atakayopenda
Ila Mtumishi Mimi nilikuwa naombi, nausikia kweli moyo wangu ukihitaji kutoa fungu la kumi lakini sina ufahamu nalo sana na nimeshangaa umetuma hilo neno kwenye group nikahisi Kama ulikuwa moyoni mwangu sasa naomba kujua tofauti ya zaka na fungu LA kumi.

No comments:

Post a Comment

KAZI KUU TANO (5) ZA IMANI KATIKA MAOMBI.

Bwana YESU atukuzwe ndugu zangu. Karibu tujifunze Neno la MUNGU. Uhusiano ni upendo unaozaa ushirikiano na mawasiliano kati ya pande m...