Thursday, 26 July 2018

MIUJIZA YA YESU INAKUFUNDISHA NINI??

HUENDA ukashangaa kujua kwamba masimulizi ya Biblia kuhusu maisha ya Yesu duniani hayatumii neno la awali la Kigiriki linalotafsiriwa kuwa “muujiza.” Maana halisi ya neno la Kigiriki (dyʹna·mis), ambalo nyakati nyingine hutafsiriwa kuwa “muujiza,” ni “nguvu.” (Luka 8:46) Linaweza pia kutafsiriwa kuwa “uwezo” au ‘kazi zenye nguvu.’ (Mathayo 11:20; 25:15) Msomi mmoja anasema kwamba, neno hilo la Kigiriki “hukazia tendo kubwa ambalo limetimizwa, na hasa nguvu zilizotumiwa kulitimiza. Tukio hilo huelezwa kuwa wonyesho wa nguvu za Mungu.”
Neno lingine la Kigiriki, (teʹras), kwa kawaida hutafsiriwa kuwa “maajabu.” (Yohana 4:48; Matendo 2:19) Neno hilo hukazia jinsi ambavyo watazamaji huathiriwa. Mara nyingi umati na wanafunzi walistaajabishwa sana na kazi zenye nguvu za Yesu.—Marko 2:12; 4:41; 6:51; Luka 9:43.
Neno la tatu la Kigiriki (se·meiʹon) linalorejelea miujiza ya Yesu linamaanisha “ishara ya nguvu kutoka kwa Mungu.” Msomi Robert Deffinbaugh anasema kwamba neno hilo “hukazia maana yenye kina zaidi ya muujiza.” Anaongeza kusema: “Ishara ni muujiza unaoeleza ukweli kuhusu Bwana wetu Yesu.”


No comments:

Post a Comment

KAZI KUU TANO (5) ZA IMANI KATIKA MAOMBI.

Bwana YESU atukuzwe ndugu zangu. Karibu tujifunze Neno la MUNGU. Uhusiano ni upendo unaozaa ushirikiano na mawasiliano kati ya pande m...