Wednesday, 26 July 2017

PUMZI YA MWANADAMU NI TAA YA MUNGU.



Je! Ni wapi uwezapo kutenda dhambi na Mungu asikuone? Je! Waweza kuishi pasipo kuvuta pumzi?

Biblia Takatifu inasema kwamba;


"Pumzi ya mwanadamu ni taa ya BWANA; Hupeleleza yote yaliyomo ndani yake." (Mithali 20:27)

Mpendwa; kila unapopumua Mungu anakuona, hata ujifiche gizani bado tu Mungu anakuona; Je, ni nani awezaye kuishi bila kupumua? Kila uvutapo pumzi, Mungu anakuona; na kupitia hiyo pumzi yako Mungu anapeleleza mambo yote ufanyayo.

Jitahidi kila wakati unatenda mambo yampendezayo Mungu.

No comments:

Post a Comment

KAZI KUU TANO (5) ZA IMANI KATIKA MAOMBI.

Bwana YESU atukuzwe ndugu zangu. Karibu tujifunze Neno la MUNGU. Uhusiano ni upendo unaozaa ushirikiano na mawasiliano kati ya pande m...